Vipimo asilia vya Kiswahili ni vipimo vya kihistoria vilivyotumiwa na Waswahili kwenye mwambao wa Afrika ya Mashariki katika karne kabla ya ukoloni na vinavyotumika hadi leo kutegemeana na mazingira.
Kwa jumla nafasi yake mara nyingi imechukuliwa na vipimo sanifu vya kimataifa kama mita na gramu, wakati mwingine pia na vipimo vya Kiingereza kama futi au inchi.